Search This Blog
Wednesday, December 11, 2019
Kenya: Gavana Sonko Aachiwa Kwa Dhamana na Masharti Magumu
Mahakama jijini Nairobi imemuachia kwa dhamana Gavana wa Nairobi, Mike Sonko aliyetiwa mbaroni siku 5 zilizopita huku akipewa masharti ya kutokwenda ofisini.
Dhamana yake ametakiwa kulipa Ksh. Milioni 15 pesa tasilimu au kuweka bondi vitu vyake vyenye thamani ya Ksh. Milioni 30.
Hapo awali gavana huyo anayeshtakiwa kwa makosa zaidi ya 30 yakiwemo ya utakatishaji fedha na rushwa, aliomba kuachiwa akieleza nafasi yake kwenye jamii na kueleza kuwa anahitaji matibabu.
Aidha Mahakama imemtaka Sonko kutotumia ofisi yake na endapo atahitaji vitu vyake ofisini atasindikizwa na maafisa upelelezi lakini pia hatakiwi kusema lolote kuhusu kesi hiyo kwenye mitandao ya kijamii.
Mfungwa afariki baada ya kupewa msamaha wa Rais
Halikadharika Mahakama imemtaka kukusanya nyaraka zake za kusafiria na kumtaka kuzuia mashabiki wake kutozua vurugu wakati kesi yake inaposikilizwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment