Search This Blog
Thursday, December 26, 2019
Ethiopia yarusha Satalaiti yake ya kwanza anga za mbali
Ethiopia imerusha satalaiti yake ya kwanza katika anga za mbali na kujiunga na nchi kadhaa za Kiafrika ambazo zina miradi ya anga za mbali kwa malengo ya ustawi na sayansi
Maafisa wa ngazi za juu wa serikali ya Ethiopia walikusanyika katika kituo cha Anga za Mbali cha Entoto karibu na mji mkuu Addis Ababa ili kutizama mubashara satalaiti hiyo inayojulikana kwa jina la ETRSS-1, ikirushwa katika anga za mbali kutoka katika kituo kimoja cha kurusha satalaiti nchini China.
Naibu Waziri Mkuu wa Ethiopia, Demeke Mekonnen amezungumza baada ya kushuhudia satalaiti hiyo ikirushwa katika anga za mbali na kusema: "Huu ni msingi wa safari yetu ya kihistoria ya kuelekea katika ustawi."
Solomon Belay, Mkurugenzi wa Taasisi ya Sayansi ya Anga za Mbali Ethiopia amesema satalaiti hiyo imeundwa kwa ushirikiano wa wahandisi wa China na Ethiopia huku serikali ya China ikichangia dola milioni 6 kati ya milioni saba zilizohitajika kuunda satalaiti hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment