Search This Blog
Thursday, December 19, 2019
Cristiano Ronaldo aacha watu vinywawazi kwa muda aliokaa hewani na kufunga bao la kichwa
Mchezaji hatari wa klabu ya Juventus, Cristiano Ronaldo aliwaacha wadau, mashabiki na wapenzi wa soka ulimwenguni vinywa wazi baada ya kufunga bao hatari na lililozua gumzo mitandaoni kwenye ushindi waliyopata wa magoli 2 – 1 dhidi ya Sampdoria Jumatano usiku.
Ronaldo akifunga bao hilo dakika 45 za kipindi cha kwanza kupitia kichwa, na kuzua gumzo kutokana na umbali alioruka hewani mpaka kuupata mpira.
Kocha wa timu pinzani, Claudio Ranieri alikaririwa akisema kuwa kwenda hewani kule na kuchukua muda mrefu mpaka kurudi chini ni 'Style za NBA' akimaanisha ndiyo wachezaji pekee wanao ruka juu mno wakati wakitaka kuingiza mpira wavuni.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 34, kupitia bao hilo anafikisha jumla ya magoli 10 akiwa wa pili kwenye mbio za kuwania ufungaji bora Serie A nyuma ya Ciro Immobile mwenye magoli 17.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment