Search This Blog
Thursday, November 28, 2019
Tanzania yaporomoka viwango vya FIFA
Tanzania imeshuka kwa nafasi moja katika viwango vya ubora wa soka duniani vilivyotolewa na FIFA hapoNovemba 28,2019, kutoka nafasi ya 133 na sasa inashika nafasi ya 134.
Kushuka kwa Tanzania kunajiri baada ya taifa hilo kupoteza 2-1 kwa Libya katia kundi J
Kwa upande mwingine Sare 1-1 dhidi ya Misri katika michuano ya kufuzu kwa kombe la mataifa mabingwa Afrika 2021 imeisaidia Kenya kupanda nafasi mbili juu katika orodha mpya za shirika hilo la kandanda duniani iliotolewa siku ya Alhamisi.
Katika orodha hiyo nayo Burundi ikishuka nafasi nane chini hadi nafasi ya 151.
Harambee Stars ya Kenya sasa ipo katika nafasi ya 106 duniani ikiwa ni nafasi mbili juu kutoka nafasi ya 108 ambayo ilikuwa ikishikilia wakati wa orodha ya miwsho iliofanyika Oktoba 24.
Timu hiyo ingepanda juu zaidi katika orodha hiyo iwapo wangepata matokeo mazuri dhidi ya Togo nyumbani katika mechi yao ya pili ya kufuzu.
Majirani Uganda hatahivyo wamepanda juu nafasi mbili zaidi hadi nafasi 77 na inasalia timu inayoorodheshwa juu zaidi huku Kenya ikiwa ya pili.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment