Search This Blog
Saturday, November 16, 2019
Jeshi la Polisi Lamshikilia Halima Mdee....Kufikishwa Mahakamani Jumatatu
Mbunge wa Kawe Halima Mdee anashikiliwa na Polisi katika kituo cha Oysterbay, kufuatia agizo la Mahakama ya Kisutu la kukamatwa kwa wabunge wanne wa CHADEMA.
Jeshi la Polisi Kinondoni limesema Mdee ameripoti mwenyewe kituoni hapo leo Novemba 16, 2019 na atafikishwa mahakamani siku ya Jumatatu.
'Ni kweli yupo hapa kituoni tunamshikilia kama ambavyo Mahakama iliagiza na yeye amekuja mwenyewe kuripoti hapa, hivyo taratibu zote za kipolisi zinafanyika na Jumatatu atafikishwa mahakami', amesema Msaidizi wa RPC Kinondoni.
Amri hiyo ya kukamatwa kwa wabunge hao Halima Mdee, Peter Msigwa, John Heche na Ester Bulaya, ilitolewa jana, Novemba 15, 2019 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo Thomas Simba, ambapo alisema kuwa kesi hiyo ilifikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya upande wa mashtaka kumhoji Mbowe na baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake kutoka upande wa utetezi na ndipo ilipobainika washtakiwa hao wanne kutokuwepo mahakamani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment