Search This Blog
Thursday, November 21, 2019
Dawa za kusisimua misuli zawaponza Maafisa wa riadha Russia
Kitengo cha Maadili cha Shirikisho la Riadha Duniani (AIU) jana kimeliadhibu Shirikisho la Riadha la Russia (RUSAF) kwa kukiuka sheria za matumizi dawa za kusisimua misuli ikiwemo kuzuia uchunguzi.
Adhabu hiyo inahusiana na mwenendo waliouonesha maafisa waandamizi wa RUSAF wakati wa uchunguzi dhidi ya mwanariadha wa kuruka juu wa Russia Danil Lysenko kwa kutotaja mahali alipo.
Rais wa RUSAF Dmitry Shlyakhtin na mkurugenzi mtendaji Alexander Parkin, mwanariadha na kocha wake wote wamefungiwa kwa muda.
Gazeti la Uingereza Sunday Times lilitoa habari mwezi Septemba likidai maafisa wa RUSAF walighushi nyaraka za kuonesha kwamba Lysenko ambaye ni mshindi wa medali ya fedha mwaka 2017 alikuwa mgonjwa sana hivyo hakuweza kusema mahali alipo baada ya kushindwa kupatikana wakati wa kuchukuliwa vipimo vya matumzi dawa za kusisimua misuli kwaajili ya mashindano.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment