Search This Blog
Wednesday, October 16, 2019
Wananachi watakiwa kuacha matumizi holela ya dawa
Jamii imetakiwa kuacha matumizi holela na yasiyosahihi ya dawa za binadamu ambapo husababisha usugu wa vimelea vya wadudu wa magonjwa katika mwili.
Akizungumza katika mkutano wa wataalamu wa afya kutoka katika nchi mbalimbali wakijadili mnyororo wa dawa na vifaa tiba, Mfamasia Mkuu wa Serikali Dkt. Daudi Msasi amesema kuwa kupunguza kiwango cha dawa ama kuongeza katika dozi husika kunachangia usugu katika miili na hivyo kusababisha dawa kushindwa kufanya kazi pale ugonjwa unapojitokeza tena.
Aidha, Dkt.Msasi amesema kuwa Serikali inaendelea kufanya maboresho katika ugavi wa dawa na vifaa tiba kwa kuainisha dawa muhimu ambapo zahani ni dawa 30 na hospitali ni dawa 312 huku madaktari wakitakiwa kufuata miongozo iliyopo ya matibabu.
“Dunia inapambana na usugu wa wadudu wa vimelea vya magonjwa yanasosababishwa na dawa na hii inasababishwa na kutumia dawa kiholela aidha chini ya kiwango ama juu ya kiwango”.
Naye Afisa uhusiano wa Shirika la umoja wa Mataifa (UNFPA) Bw.Bright Wallen amesema kuwa UNFPA wamekuwa wakishirikiana na Serikali katika kutoa dawa na vifaa tiba pamoja na kusaidia kutibu watu.
“Takribani wadau 300 wamehudhulia mkutano huu wakijifunza mada mbalimbali zimekuwa zikitolewa na kujifunza na lengo kuu kuona ni namna gani wanaweza kuboresha mfumo wa dawa kwenye masuala ya ugavi”.Amesema Bw. Wallen.
Kwa upande wao baadhi ya wadau waliohudhuria mkutano huo akiwemo Bw. John mvutakamba amesema kuwa mkutano huo utaweza kufanya tathimini ya huduma za afya hususani katika ugavi hivyo kuweza kuanisha changamoto na kuweza kuunda mbinu za kutatua.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment