Uongozi wa klabu ya Mtibwa Sugar hadi sasa upo njia panda kufuatia kufungiwa kwa viwanja vyake vyote ilivyokuwa inachezea mechi za nyumbani kunako Ligi Kuu Bara.
Ikiwa ni wiki kadhaa tangu kufungiwa Uwanja wa Manungu, Mtibwa ilipangiwa kutumia uwanja wa Jamhuri ambao nao wiki hii umetangazwa kufungiwa na Bodi ya Ligi.
Saleh Jembe ilizungumza na Ofisa Habari wa Mtibwa, Thobias Kifaru, ambaye aliibuka na kusema kuwa hadi sasa wapo njia panda kuwa watatumia uwanja gani.
"Kiukweli hatujajua maana Manungu ilifungiwa na sasa Jamhuri nayo pia imefungiwa.
"Tunachoomba sisi TFF na Bodi ya Ligi waturuhusu tutumia huu wa Manungu sababu tunaingia kwenye gharama kubwa sana kupeleka timu Jamhuri, inakuwa kama tunaenda ugenini.
"Tunawaomba TFF watusaidie kwa hili hata kwa kipindi hiki tukiwa tunaelekea kujenga uwanja wetu wenyewe."
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment