Search This Blog
Thursday, October 24, 2019
Mama Salma Kikwete aungana na Wanawake Viongozi katika Mkutano wa Kimataifa Burundi
Mke wa Rais Mstaafu ambaye pia ni Mbunge wa Kuteuliwa, Mama Salma R Kikwete ameungana na Wanawake Viongozi mbalimbali kutoka Afrika katika Mkutano wa Kimataifa wa Wanawake Viongozi unaofanyika nchini Burundi kuanzia tarehe 24-26 Octoba 2019
Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) anashiriki Mkutano huo wa siku 3 ambao umeanza Oktoba 24 na kufunguliwa na Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza.
Mkutano huu umehudhuriwa na Mke wa Rais wa Burundi mwenyeji muandaaji Mama Denise NKURUNZIZA, Naibu Rais wa pili wa Bunge la nchi, Jocky Chantal NKURUNZIZA, na Kaimu Balozi wa Tanzania Nchini Burundi, Dr. Edmud Juma Kitokezi.
Viongozi wengine ambao wamehudhuria Mkutano huu ni pamoja na Naibu Karibu Mkuu UN anayeshughulikia maswala ya Afrika Mama Bintou Keita , Mke wa Rais wa Congo Brazaville Mama Antoinette Sassau Nguess. Mke wa Rais wa Central Africa Republic Madam Brigette Touadera.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...



No comments:
Post a Comment