Search This Blog
Thursday, October 24, 2019
China kuandaa michuano ya kwanza ya Kombe la Dunia kwa vilabu
Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Gianni Infantino jana alitangaza kuwa China itaandaa michuano ya kwanza ya Kombe la Dunia la Klabu lililoongezwa timu 24 na kusifu kuwa ni uamuzi wa kihistoria.
Akitoa tangazo hilo baada ya mkutano wa Baraza la FIFA huko Shanghai, Infantino amesema mashindano yatafanyika Juni na Julai mwaka 2021.
Hakutoa ufafanuzi zaidi lakini amesema mashindano yatakuwa na timu nane kutoka Ulaya, moja kutoka China, moja kutoka Oceania na tatu kutoka mashirikisho ya bara jingine. Infantino amethibitisha kuwa China, ambayo imefanya soka kuwa kipaumbele cha taifa chini ya rais Xi Jinping, imekuwa mgombea pekee.
Amesema vigezo vya kuchagua timu vitaamuliwa katika wiki chache zijazo, lakini Atletico Madrid, Real Madrid, Chelsea na Liverpool watashiriki kwa vile hizo ni timu nne washindi wa makombe ya Ulaya.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...

No comments:
Post a Comment