Search This Blog

Sunday, October 13, 2019

Kishindo cha JPM, Ahamia Rasmi Dodoma



Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo amehamia rasmi Jijini Dodoma na kwenda kujiandikisha kwenye daftari la orodha ya wapigakura katika kituo cha Sokoine kitongoji cha Sokoine wilayani Chamwino.

UWT yasisitiza madaraka 50 kwa 50
Akizungumza na wananchi waliokuwepo kwenye kituo cha kujiandikishia, Rais Magufuli amesema ameshahamia rasmi makao makuu ya nchi na kuwaahidi wananchi wa Chamwino kuwa tatizo la maji walilonalo litafanyiwa kazi haraka.

” Nimehamia rasmi Dodoma, nimejiandikisha katika eneo langu na nitapiga kura hapa hapa tarehe 24 kuwachagua viongozi wangu wa mtaa” amesema Rais Magufuli.


Ikumbukwe kuwa mwaka 2016 Serikali ya awamu ya tano ilihamia rasmi jijini Dodoma na Aprili 2019 Rais Magufuli alizindua mji mpya wa Serikali, ambao ndiyo makao makuu ya wizara zote.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...