Kiasi wakaazi 940,000 wa jimbo la California nchini Marekani wataathirika na kuzimwa kwa huduma za umeme kufuatia upepo mkali kutishia kuangusha nyaya na kusambaza zaidi moto unaoendelea kuwaka kaskazini ya California.
Taarifa iliyotolewa na mamlaka ya nishati ya California imesema hali ya mbaya ya hewa ya upepo mkali inayotajiwa inaleta kitisho katika mfumo wa usambazaji umeme.
Mamlaka hiyo imesema umeme utakatwa kwa awamu katika wiliya zote 36 za jimbo hilo kuanzia siku ya Jumamosi hadi mchana wa kesho Jumatatu. Gavana wa California Gavin Newsom amesema kiasi dola milioni 75 ili kuwasaidia wale watakaoathirika na katizo la huduma za umeme.
Moto mkubwa wa msituni unaendelea kuwaka kaskazini ya California umelazimisha zaidi ya wakaazi 50,000 kuamriwa kuondoka na hali ya upepo mkali unatishia kusambaza zaidi moto huo.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment