Search This Blog
Thursday, October 3, 2019
Chadema Yajitetea Kutofanya UCHAGUZI...Yasema Kamati Ilibadilisha RATIBA ya Uchaguzi
Kutokana na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kukiandikia barua Chama cha Demokrasia na Maendeleo kuhusu Uchaguzi, Chama hicho kimesema Katiba ya Chama, Ibara ya 6.3.3 (a) inatoa mamlaka kwa Kamati Kusogeza mbele uchaguzi mkuu wa ndani ya chama
Taarifa yao inaeleza kuwa, Kamati Kuu ya Chama ilikaa kikao Julai 27 na 28, 2019, na kurekebisha ratiba ya uchaguzi ambapo utakamilika mwezi Desemba kwa ngazi ya Taifa
Aidha, chama hicho kimeeleza kuwa katika hatua ya sasa, kinaifanyia kazi barua hiyo ili iweze kuifikia Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ndani ya muda husika uliotajwa
Wakati huo huo, kimewahakikishia Viongozi wake, wanachama na Watanzania wote wapenda demokrasia na mabadiliko kuwa hakijakiuka Sheria ya Vyama vya Siasa nchini wala Katiba ya Chama katika mwenendo wa shughuli zake
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment