Search This Blog

Thursday, October 24, 2019

Bangladesh: Waliomchoma moto mwanafunzi wahukumiwa kifo


Mahakama nchini Bangladesh imewahukumu kifo watu 16 waliomchoma moto hadi kufa mwanafunzi aliyetoa taarifa ya mwalimu mkuu wake kumnyanyasa kingono.

Nusrat Jahan Rafi, 19, aliyefariki mwezi Aprili mwaka huu katika mji wa Feni, nje ya mji mkuu wa Dhaka nchini humo, aliuawa kwa kuchomwa moto baada ya kutoa taarifa ya kunyanyaswa kingono na mwalimu mkuu wa shule aliyokuwa akisoma.

Mwalimu mkuu aliyetuhumiwa na Nusrat kwa unyanyasaji na wanafunzi wengine wawili wa kike ni miongoni mwa waliohukumiwa adhabu hiyo ya kifo.

Mara baada ya taarifa ya kifo cha binti huyo kusambazwa, ziliamsha mfululizo wa maandamano nchi nzima yaliyokuwa na lengo la kushinikiza Nusrat apate haki.

Walimu watatu wakiwemo mwalimu mkuu, Siraj Ud Doula, ambaye polisi inasema alitoa amri ya kuuwa kwa mwanafunzi huyo akiwa jela baada ya kukamatwa, walipatikana na hatia ya mauaji hayo pia.

Wengine waliopatikana na hatia ni pamoja na Ruhul Amin na Maksud Alam, kiongozi wa Chama Tawala cha Awami League. Maofisa kadhaa wa polisi nao walipatikana na hatia ya kushirikiana na wale waliokamatwa kueneza taarifa za uongo kwamba Nusrat alijitoa uhai.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...