Search This Blog
Tuesday, October 15, 2019
Akamatwa na Polisi kwa kujiandikisha mara mbili kwenye daftari la Wapiga Kura
Mkazi wa Kasanga Manispaa ya Morogoro, Ngeze Mwagilo (29) anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kujiandikisha mara mbili katika daftari la wapigakura kwenye vituo viwili tofauti ndani ya manispaa ya Morogoro.
Akizungumza na Waandishi wa Habari hapo jana Kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Wilibroad Mutafungwa alisema kuwa mtu alikamatwa baada ya jeshi hilo kupata taarifa na kumfuatilia mtuhumiwa huyo wakati wa shughuli ya uandikishaji ikiendelea.
Mtuhumiwa huyo anadaiwa kujiandikisha katika kituo cha Kasanga kata ya Mindu na baadaye kwenda kujiandikisha katika kituo cha kiwanja cha Ndege kata ya Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro.
Ameongeza kuwa mtuhumiwa huyo anaendelea kuhojiwa na atafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi kukamilika ili sheria ichukue mkondo wake.
Mutafungwa amewatahadharisha wananchi mkoani humo wenye lengo la kutaka kuvuruga shughuli hiyo watachukuliwa hatua za kisheria kuwa polisi itahakikisha inawakamata huku akiwataka kuacha kufanya uhalifu huo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment