Search This Blog

Wednesday, September 18, 2019

Wananchi Nyamongo wafanyiwa tathimini ya fidia kupisha ujenzi bwawa la maji taka


Serikali imeanza kusikiliza kilio cha muda mrefu cha wananchi wa Nyamongo katika wilaya ya Tarime mkoani Mara kwa kuanza kufanya tathmini ya fidia ya kutwaa eneo la ardhi kwa ajili ya kupanua Mgodi wa Dhahabu wa ACACIA North Mara ili kujenga Bwawa la Maji Taka.

Tayari timu ya wataalamu 25 kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi inayojumisha Ofisi ya Mthamini Mkuu wa Serikali pamoja na idara ya Upimaji na Ramani iko eneo la Nyamongo kijiji cha Matongo wilaya ya Tarime mkoani Mara kutathmini mali za wananchi ili kulipwa fidia na kupata eneo kwa ajili ya ujenzi wa Bwawa la Maji Taka.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo jana katika kijiji cha Matongo wilaya ya Tarime mkoa wa Mara Mthamini Mkuu wa Serikali Evaline Mugasha alisema, zoezi la uthamini linalofanyika ni kwa ajili ya kutwaa eneo la ujenzi wa Bwawa la Maji Taka katika eneo la Nyamongo lenye ukubwa wa hekta 237 ambalo linahusisha vitongoji vitatu vya Kigonga A, Kwinyunywi na Kigonga B ambapo uthamini wake ulishaanza toka mwezi julai mwaka huu.

Mugasha alisema, uthamini huo unaangalia mali inayohamishika na ile isiyohamishika na kufuata sheria ya ardhi na ile ya kijiji na kusisitiza uthamini huo umekuwa ukifanyika kwa uwazi na hauna lengo la kumnufaisha au kumpunja mtu yeyote.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...