Search This Blog
Wednesday, September 18, 2019
Wananchi Nyamongo wafanyiwa tathimini ya fidia kupisha ujenzi bwawa la maji taka
Serikali imeanza kusikiliza kilio cha muda mrefu cha wananchi wa Nyamongo katika wilaya ya Tarime mkoani Mara kwa kuanza kufanya tathmini ya fidia ya kutwaa eneo la ardhi kwa ajili ya kupanua Mgodi wa Dhahabu wa ACACIA North Mara ili kujenga Bwawa la Maji Taka.
Tayari timu ya wataalamu 25 kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi inayojumisha Ofisi ya Mthamini Mkuu wa Serikali pamoja na idara ya Upimaji na Ramani iko eneo la Nyamongo kijiji cha Matongo wilaya ya Tarime mkoani Mara kutathmini mali za wananchi ili kulipwa fidia na kupata eneo kwa ajili ya ujenzi wa Bwawa la Maji Taka.
Akizungumza wakati wa zoezi hilo jana katika kijiji cha Matongo wilaya ya Tarime mkoa wa Mara Mthamini Mkuu wa Serikali Evaline Mugasha alisema, zoezi la uthamini linalofanyika ni kwa ajili ya kutwaa eneo la ujenzi wa Bwawa la Maji Taka katika eneo la Nyamongo lenye ukubwa wa hekta 237 ambalo linahusisha vitongoji vitatu vya Kigonga A, Kwinyunywi na Kigonga B ambapo uthamini wake ulishaanza toka mwezi julai mwaka huu.
Mugasha alisema, uthamini huo unaangalia mali inayohamishika na ile isiyohamishika na kufuata sheria ya ardhi na ile ya kijiji na kusisitiza uthamini huo umekuwa ukifanyika kwa uwazi na hauna lengo la kumnufaisha au kumpunja mtu yeyote.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment