Search This Blog

Wednesday, September 18, 2019

Ofisi ya Klabu ya riadha Babati,Garmaa Athletic kufunguliwa wikiendi hii


Na John Walter-Babati

Mashindano ya riadha ya kwa rika zote yanatarajiwa kufanyika tarehe 21.9.2019 Mjini Babati katika uwanja wa Kwaraa katika Mita 2.5, Kilomita 5 na Kilomita 10 ikiwa ni sambamba na ufunguzi wa Ofisi ya Garmaa Athletic  Club.               

Akizungumza na Muungwana Blog Mkurugenzi wa taasisi ya ‘Garmaa Athletic  ’ inayoandaa mashindano hayo, Abdalah Magubika, alisema wameamua kuandaa mashindano hayo ili kukuza mchezo wa riadha kwa mkoa wa Manyara na kuzindua rasmi ofisi hizo ili kuendelea kuupa heshima Mchezo huo hapa nchini.

Alisema mbio hizo ni moja ya chachu ya kuwaandaa wanariadha wengine wa baadae watakaoipeperusha vyema bendera ya Tanzania kama ilivyo kwa akina Alphonce Simbu na wengine.

Alisema mchezo wa riadha kwa sasa unakuwa kwa kasi kubwa ukichagizwa na wanariadha maarufu kutoka katika mkoa wa Manyara.

Kuhusu Maandalizi Magubika , amesema mpaka sasa yanaendelea vizuri hivyo yataanza saa 1:00 asubuhi hadi majira ya mchana.

Hata hivyo amewashukuru wadau wa Michezo  waliojitokeza kutoa michango yao ili kuhakikisha mbio hizo zinafanikiwa kufanyika.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...