RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kufungua Tamasha utamaduni na Sanaa JAMAFEST la nchi za Afika Mashariki jijini Dar es Salaam.
Tamasha lenye lengo la kuunganisha nchi za Afrika Mashariki kupitia sanaa na utamaduni litazinduliwa jijini Dar es Salaam Septemba 22,2019 katika uwanja wa Taifa jijini.
Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hasan Abbas amesema wakati akizungumza na waandishi wa habari wakati wa semina ya kuwajengea Uwezo kwajili ya kulipoti na kutoa taarifa mbalimali za Tamasha la Jamafest leo jijini Dar es Salaam.
Amesema kuwa tamasha hilo la Utamaduni na sanaa la Jumuiaya ya Afrika Mashariki litatanguliwa na matembezi ya
litazinduliwa Jumapili na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.John Magufuli kuanzia saa nane katika viwanja vya Taifa jijini Dar es Salaam.
Amasema tamasha hili litakalohusisha nchi za jumuiya ya Afrika mashariki litafanya maonesho ya utamaduni wa nchi za Afrika Mashariki ambapo kila nchi itaonesha sanaa na tamaduni zao.
Nae Mwenyekiti wa maandalizi wa tamasha la Jamafest, Joyce Fisoo amasema kuwa tamasha hilo litahudhuliwa na washiriki kutoka Kenya 612, Uganda 201, Burundi 179, Rwanda 125 na zaidi ya watanzania elfu moja kuhudhulia tamasha hilo.
No comments:
Post a Comment