Search This Blog
Saturday, September 7, 2019
Papa alaani rushwa ya kimataifa
Akikamilisha ziara yake ya siku mbili nchini Msumbiji, kiongozi wa Kanisa Katoliki ulimwenguni, Papa Francis, amekosoa rushwa inayofungamanishwa na misaada ya maendeleo.
Licha ya utajiri mkubwa wa mali ghafi, wananchi wengi wa nchi hiyo ya kusini mashariki mwa Afrika wanaishi katika hali ya umaskini uliokithiri, amesema kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki ulimwenguni katika misa katika mji mkuu Maputo.
Amelaani mitindo ya kufungamanishwa masilahi ya kiuchumi ya mataifa tajiri kiviwanda na misaada ya maendeleo.
Amesema mitindo hiyo inatoa picha kana kwamba wale wanaojidai wanataka kusaidia, kimsingi wanafuata masilahi mengine.
Kiongozi wa kanisa katoliki ulimwenguni Papa Francis anatarajiwa kuondoka Maputo kuelekea Antananarivo-Madagascar-kituo cha pili cha ziara yake hiyo itakayomfikisha pia kisiwani Mauricius.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment