Search This Blog
Tuesday, September 17, 2019
IGP Sirro afanya mabadiliko kwa Ma-RPC
Mkuu wa Jeshi Polisi nchini Tanzania (IGP), Simon Sirro amefanya mabadiliko madogo ya
makamanda wa polisi wa mikoa (RPC).
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, David Misime amesema katika mabadiliko hayo Wilbroad Mutafungwa amehamishiwa makao makuu akitoka Morogoro. Misime amesema nafasi ya Mutafungwa imechukuliwa na Hamisi Issa aliyekuwa Kilimanjaro.
Ameongeza kuwa Saidi Hamdani aliyekuwa Njombe amehamishiwa Kilimanjaro na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Geita, Daniel Sillah anakwenda kuwa Kamanda wa Polisi Njombe.
“Mabadiliko haya ni ya kawaida katika kuboresha utendaji kazi wa jeshi la polisi,” amesema Misime Ingawa pia amesema mabadiliko hayo ni ya kawaida lakini huenda kwa Kamanda wa Polisi wa Morogoro yamefanyika ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa aliyoyatoa Bungeni jijini Dodoma.
Ikumbukwe Septemba 13, 2019 wakati akiahirisha mkutano wa 16 wa Bunge la 11 hadi Novemba 3,2019 Bungeni jijini Dodoma, Majaliwa alisema kamati aliyoiunda kuchunguza ajali ya lori la mafuta ya petroli iliyotokea Agosti 10, 2019 mkoani Morogoro imekamilisha shughuli yake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta ya Ujenzi, Arch. Elius Mwakalinga, akitoa maelekezo kwa Kai...

No comments:
Post a Comment