Search This Blog
Wednesday, September 11, 2019
Dkt. Ndugulile ataka maboresho ya mifumo ya takwimu
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ametaka maboresho ya mifumo ya takwimu za tafiti mbalimbali zinazofanyika nchini.
Dkt. Ndugulile amesema hayo wakati akizindua kongamano linalohusisha wadau mbalimbali wa masuala ya UKIMWI ambao wanawasilisha tafiti na takwimu mbalimbali ambazo zinaendelea kufanyiwa kazi nchini.
“Tunahitaji tuboreshe mifumo yetu ya takwimu ili tuwe na uwiano wa takwimu ambazo zinawasilishwa katika mkutano huu, hapa nimeona takwimu mbalimbali zimewasilishwa, ninaomba takwimu hizo ziwe za wote kwa sababu tuna wadau wengi wanaoshiriki katika mapambano haya dhidi ya Ugonjwa wa UKIMWI hivyo maelekezo yangu kuwe na mfumo mmoja wa takwimu ambao kila mmoja atakua anachangia takwimu zake na mfumo huo uwe wa mwisho utakaotoa takwimu za wote”. Amesema Dkt. Ndugulile.
Hata hivyo Dkt. Ndugulile amehamashisha makongamano kama hayo yafanyike mara kwa mara ili kuwawezesha wanazuoni, watunga sera na walengwa kukaa pamoja ili kujadiliana mambo mbalimbali ambayo yanahusuana na afua ambazo zinatekelezwa hapa nchini.
Kongamano hilo limeshirikisha taasisi za Serikali ambazo ni NIMR na TACAIDS pamoja na wadau mbalimbali wanaofanya tafiti kuhusiana na ugonjwa wa UKIMWI ambao wamekutana ili kuwasilisha takwimu za tafiti mbalimbali ambazo wanazifanyia kazi katika maeneo yao.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment