Search This Blog

Saturday, September 7, 2019

DC Muro agusa maisha ya Walemavu


Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muro kwa kushirikiana na Taasisi ya walemavu wa Uti wa mgongo KASI imetoa misadaa mbalimbali kwa walemavu wenye matatizo ya Uti wa Mgongo walioko katika wilaya ya Arumeru.


Dc Muro ambae ameamua kuonyesha juhudi binafsi katika kuwasaidia watu wenye ulemavu amesema wametoa misaada ya kuanza maisha ya Ujasiriamali kwa watu wenye ulemavu ili waweze kumudu maisha hatua itakayowasaidia kuwaondoa katika kundi la utegemezi katika familia.

Huku akisema jambo linalochangia watu kuwanyanyapaa ambapo ametoa misaada mbalimbali ya kuanzisha biashara ndogondogo ikiwemo uuzaji wa vifaa vya ujenzi, vyombo vya majumbani, miradi ufugaji kuku, miradi ya ufugaji mbuzi na miradi ya uuzaji maji ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono serikali ya awamu ya tano chini ya Mhe, Rais, Dkt. John Pombe Magufuli

Aliongeza kusema kuwa kwa kuendelea kuwajali watu wenye ulemavu hatua inayowasaidia kuwajengea uwezo wa kupambana na changamoto walizonazo ambazo zinawafanya kuwa tegemezi kwenye jamii.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...