Search This Blog
Tuesday, September 3, 2019
Bunge Lafanya Azimio La Kumpongeza Rais Magufuli Kwa Kuchaguliwa Kuwa Mwenyekiti SADC
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Leo Sept.3,2019 limefanya azimio la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli baada ya hivi Karibuni kupewa nafasi ya kuwa Mwenyekiti wa Bunge la Jumuiya Ya Madola Afrika SADC.
Mwenyekiti kamati ya Bunge ya Mambo ya nje na Usalama Mhe. Musa Azan Zungu amesema Waasisi wa Jumuiya ya maendeleo nchi wanachama wa Kusini Mwa Afrika wamefanya makubwa ikiwa ni pamoja na kuunganisha nchi wanachama hivyo matamanio ya waasisi hao ikiwa ni pamoja na Rais wa awamu ya Kwanza Mwl.Julius Kambarage Nyerere na Aman Abeid Karume yanatimizwa na Rais Magufuli katika kusukuma mbele maendeleo .
Nao baadhi ya Wabunge wamesema kuchaguliwa kwa Rais Magufuli kuwa Mwenyekiti wa SADC itasaidia kuondoa kuritimba wa masoko katika biashara huku pia wakisema kuwa Tanzania ni Kitovu cha Cha Ukombozi kwa nchi wanachama wa SADC katika kupigania Uhuru.
Akihitimisha katika Azimio hilo la Pongezi bungeni jijini Dodoma Mhe.Zungu amesema ili Nchi wanachama wa SADC kujikomboa lazima kwanza kutafuta masoko ya ndani
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment