Search This Blog

Monday, September 16, 2019

Azam FC kuifuata Triangle United kwa mtindo huu


Kikosi cha Azam FC kinatarajia kuondoka Septemba 22, 2019 kwenda nchini Zimbabwe kwaajili ya mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Triangle United ya huko utakaopigwa Septemba 28, 2019.

Afisa Habari wa timu hiyo Jaffer Idd Maganga amesema timu hiyo itaondoka kwa mafungu ambapo kundi la kwanza litahusisha wachezaji ambao hawatakuwa kwenye majukumu ya timu ya taifa (Taifa Stars) itakayokuwa dimbani Septemba 21 kukabiliana na Sudan katika mchezo wa kufuzu CHAN.

Kundi lingine litaondoka Septemba 23 likihusisha wachezaji waliokuwa kwenye majukumu ya timu ya taifa pamoja na kocha Etienne Ndayiragije ambaye pia anakaimu nafasi ya kocha mkuu wa timu hiyo ya taifa.

Katika hatua nyingine uongozi wa Azam FC umewashukuru Watanzania wote kwa umoja waliouonesha na kuujaza uwanja wa Chamazi katika mchezo wa kwanza huku ukiomba radhi kwa matokeo mabaya.

“Tunajua tumewaangusha sana Watanzania kiujumla kwa aina ya matokeo tuliyopata, lakini haikuwa nia yetu, bali ni sehemu ya matokeo ya soka," alisema.

Huu sio mwisho wa vita, ndiyo kwanza dakika 90 za mwanzo zimemalizika, tumegundua tulipoteleza na sasa tumeanza kujipanga vilivyo kuelekea dakika 90 nyingine zijazo ugenini”.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...