Search This Blog
Tuesday, August 6, 2019
UGANDA: Bobi Wine kuburuzwa mahakamani kwa tuhuma za kumkera na kumkejeli Rais Museveni
Msanii wa muziki nchini Uganda, Robert Kyagulanyi maarufu maarufu kwa jina la Bobi Wine ameshtakiwa nchini humo kwa tuhuma za kumkera na kumkejeli Rais wa taifa hilo, Yoweri Museveni.
Mashtaka hayo, Yanajumuishwa na tukio la Agosti mwaka Jana, Ambapo Bobi Wine alishutumiwa kuongoza maandamano sehemu ambayo gari la Rais Museveni lilipigwa mawe na Wafuasi wa Bobi Wine.
Mbunge huyo wa Jimbo la Kyadondo Mashariki, Tayari anakabiliwa na shtaka la uhaini na anaweza kufungwa kifungo cha maisha iwapo atapatikana na hatia.
Mapema mwezi Julai mwaka huu, Bobi Wine alitangaza kuwa atawania Urais wa Uganda dhidi ya Rais Museveni katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2021.
Chanzo: Daily Monitor.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment