Search This Blog
Friday, August 9, 2019
RC Makonda aonya kuhusu Coco Beach, ‘Hii hujuma haikubaliki’
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda ametoa mwezi mmoja kwa Manispaa ya Kinondoni kuanza ujenzi wa mradi wa ufukwe wa Coco Beach, kwa kile alichokidai kuwa Manispaa hiyo imekuwa ikichelewesha mradi huo.
Ametoa agizo hilo jijini Dar es salaam, wakati alipotembelea eneo la ufukwe wa Coco Beach, ambapo amesema kuwa Manispaa hiyo imekabidhiwa Bilioni 14, lakini mpaka sasa wanaishia kufanya vikao tu.
Amesema kuwa eneo hilo la Coco Beach limerudishwa kuwa eneo la umma, ili watu waende kupumzika, na Rais Magufuli tayari alishatoa bilioni 14, ili kuanza kuijenga Coco, lakini kwa masikitiko makubwa mpaka sasa ujenzi haujaanza.
“Moja ya mambo yaliyonishangaza ni mshauri waliyempata ameacha mchoro wa bilioni 14, amekuja na mchoro wa bilioni 40, tumewapa muda wa mwezi mmoja ili Coco Beach ianze kujengwa, haiwezekani fedha imetolewa miradi haiendi, hatuwezi kukubali Rais wetu aendelee kuhujumiwa, natoa mwezi mmoja muanze kushughulikia ujenzi” amesema Makonda.
Katika ziara hiyo Makonda amewataka viongozi wa Manispaa ya Kinondoni kuendana na kasi ya ujenzi wa daraja la Selander, ambapo amependekeza mpaka mradi wa daraja hilo kukamilika na uboreshaji wa ufukwe wa Coco Beach uwe umekamilika
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment