Search This Blog
Thursday, August 29, 2019
Nikki Wa Pili Ataja Sababu za Mastaa Kudanganya Umri na Kuvimbia Mashabiki
Staa wa muziki wa HipHop rapa Nikki Wa Pili amefunguka 'issue' za mastaa kupenda kudanganya umri na kuwavimbia mashabiki katika mitandao ya kijamii.
Nikki Wa Pili amefuguka hayo baada ya kumalizika kwa mkutano uliokutanisha wasanii wote, wanahabari chini ya waziri wa habari, sanaa, utamaduni na michezo Mh. Harrison Mwakyembe.
Akizungumza na EATV & EA Radio Digital, amesema, "Sababu ni nyingi hata kibiashara pia, Mtu anaweza kukujaji kutokana na umri wako kwa hiyo ina busara zake".
Aidha Nikki Wa Pili ameeleza kuhusu kauli aliyosema ni bora mastaa wawe wanajibu maoni 'comments' za mastaa wenzao kwenye mitandao ya kijamii kuliko kujibu watu wa kawaida.
"Nilikuwa namaanisha watu ambao hawana staha, mimi ni mmoja wa wasanii wanaowasiliana na watu wengi ila watu hao wanakuwa hawana staha, kama unapenda uwasiliane na mtu lazima uwe na ustaarabu, kama hakuna ustaarabu mahusiano yatavunjika na nafikiri nimewaambia ukweli sijawavimbia" amesema Nikki Wa Pili.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment