Search This Blog
Thursday, August 29, 2019
Magari 20 ya wizi kutoka Kenya yakamatwa Tanzania
Jeshi la Polisi Mkoani Kilimanjaro, limefanikiwa kukamata magari 20 yaliyoibwa nchini Kenya mwaka 2018/2019 na kutaja wilaya nne za mkoa huo kuwa zilitumika kama uchochoro wa kuyaingiza Tanzania magari hayo.
Hayo yamesemwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Hamis Issah alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, ambapo amezitaja wilaya hizo kuwa ni Rombo, Mwanga, Same na Siha.
Amesema kuwa magari hayo 20 ya aina mbalimbali yakiwamo malori saba, yana thamani ya shilingi za Kenya 80,860,000 sawa na fedha za Tanzania Sh1.7 bilioni.
Aidha, miongoni mwa magari hayo ni Toyota Landcruiser manne, Mercedes Benz tatu, Mercedes Benz truck (lori), Toyota prado moja, Toyota Probox moja, Toyota axio moja, Toyota Allion moja, Toyota Mitsubish nne na Nissan Patrol V.8 Station wagon.
“Hatua hiyo imekuja kutokana na kuwepo kwa wimbi la wizi wa magari yanayoibiwa nchini Kenya yanayopitia mkoa wa Kilimanjaro na baadaye kwenda mikoa mingine,” amesema kamanda Issah
Aidha, amesema kuwa watuhumiwa tisa wanashikiliwa wakihusishwa na magari hayo ambapo, Polisi Kilimanjaro kwa kushirikiana na polisi wa Dar Es Salaam walifanikiwa kuubaini mtandao huo ambapo tayari watu tisa wamekamatwa jijini Dar es salaam.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment