Search This Blog
Monday, August 19, 2019
Mwalimu adaiwa kujiua kwa kunywa sumu
Mwalimu Mkuu wa Sekondari ya Mbalamaziwa iliyopo mkoani Iringa, Roida Mbalwa amefariki dunia kwa kunywa sumu baada ya kutuhumiwa kwenye mkutano na kiongozi mmoja kutumia vibaya fedha za ujenzi.
Mume wa marehemu, Sharif Utenga amesema kuwa kiongozi huyo aliitisha mkutano wa hadhara kata ya Mbalamaziwa na wananchi kueleza kuchangishwa michango mingi.
”Ninachofahamu ni kwamba alikuja kiongozi flani akazungumza na wananchi wakasema michango imekuwa mingi, ndipo hapo wakaamua kwenda kumkagua Mwalimu Roida, na baada ya ukaguzi ilibainika kuwa kuna hasara takribani milioni 200,”amesema Utenga
Aidha, Utenga amesema kuwa mara kwa mara viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Mufindi wamekuwa wakienda shuleni hapo na kukagua ujenzi kwasababu majengo hayo yanatarajiwa kuzinduliwa na Mwenge.
”Mke wamgu alikuwa akipata presha ya kazi kutoka kwa viongozi waliokuwa wakifika kukagua, walikuwa wakali na kumtuhumu kwa matumizi mabaya ya fedha, alikuwa akiwaambia waalimu wenzake kuwa ipo siku atakuja kujiua,”amesema Utenga
Hata hivyo, diwani wa Mbalamaziwa, Zubery Nyamolelo amesema kuwa mwalimu huyo hajawahi kutuhumiwa kwa lolote.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment