Search This Blog
Saturday, August 3, 2019
CUF wamlilia Rais Magufuli
Chama cha Wananchi CUF kimemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kuruhusu mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa nchini hususani katika kipindi hiki kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Mkurugenzi wa Sheria na haki za binadamu wa chama hicho, Salvatory Magafu ambapo amesema, ''tunamuomba Rais Magufuli kwa heshima na taadhima aruhusu, atoe tamko la kuruhusu mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa''.
Aidha Mkurugenzi huyo amelitaka jeshi la polisi nchini kuacha kukiuka sheria na lifanye kazi bila ubaguzi wala upendeleo ili kuendelea kulinda amani ya nchi.
Hatua hii imekuja baada ya chama hicho kuliandikia barua jeshi la polisi ya kuomba kibali cha kufanya mkutano wa hadhara Vingunguti relini, lakini baadae walipokea barua kutoka Ofisi ya Mkuu wa Polisi Buguruni ya kuzuia mkutano huo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment