Search This Blog
Wednesday, August 21, 2019
Cristiano Ronaldo afunguka mipango ya kustaafu soka
Mshambuliaji wa Juventus na timu ya taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo ameweka wazi hana mpango wa kustaafu soka mwishoni mwa msimu huu wa 2019/20 ama miaka ya hivi karibuni.
Mreno huyo mwenye umri wa miaka 34, ameimbia Fox Sports kuwa, bado na uwezo wa kuendelea kucheza soka kwa kiwango kikubwa cha ushindani hadi akifikia miaka 40.
"Sina mawazo ya kuachana na mpira, pengine naweza kuwa na mawazo hayo nikifikisha miaka 40 au 41, ninauwezo wa kuendelea kucheza. Zawadi ya kipaji nilichonacho natakiwa kuendelea kukifurahia," alisema kwenye mahojiano na kituo cha Tv, Italia.
Aliongeza; "Kuna wanasoka mwenye rekodi zaidi yangu, sidhani kama wapo ambao wanaweza kunizidi."
Ronaldo, ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia wa mwaka mara tano sawa na nyota wa FC Barcelona, Lionel Messi ambaye kwa sasa anasumbuliwa na majeraha.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment