Boti inayomilikiwa na klabu ya starehe ya Yacht jijini Tanga, imepinduka baharini jana jioni Agosti 11, 2019, ikiwa na watu 11 wengi wao wakiwa ni wafanyakazi wa Benki ya NMB Korogwe.
Akiongea na EATV&EA Radio Digital, Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi Edward Bukombe, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.
''Ni kweli ajali imetokea, na watu 10 waliokolewa na wakapata huduma ya kwanza hivyo wanaendelea vizuri. Mmoja hajapatika hadi sasa, jitihada za kumtafuta zinaendelea'', amesema Kamanda Bukombe.
Aidha Kamanda ameeleza kuwa watu hao walikuwa wamekuja kwaajili ya mapumziko ya sikukuu, hivyo wakawa wanataka kufika visiwa vya jirani na wakati wanakwenda ndio wakakumbwa na upepo mkali na walipotaka kugeuza ndio ikapinduka.
Kamanda ameongeza kuwa Boti hizo zinamilikiwa na klabu hiyo, hivyo hutoa huduma kwa wateja wao wanaotaka kufika visiwa vya karibu na eneo hilo, ambavyo haviko mbali na vinaonekana hata ukiwa mjini.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment