MWANAMUZIKI wa Bongo Fleva ambaye pia ni msanii wa filamu, Baby Madaha ameibuka na kueleza kwamba muziki wake siyo wa kiki bali anafanya muziki wa kweli hivyo asifananishwe na Amber Rutty.
Akistorisha na Amani, Baby Madaha alisema kwa sasa amekua hawezi kufanya kiki za kijinga kama Amber Rutty kwani zitamshushia hadhi hivyo amekuwa akifanya jitihada ili akubalike kwa kazi nzuri na siyo kwa kiki tena kama zamani.
“Wasanii wanaofanya kiki hasa wakiwa na ngoma mpya hao ni wafanyabiashara lakini mimi ni mwanamuziki ndiyo maana nimetoa ngoma mpya hata sijafanya kiki maana zina madhara mengi kwani kuna mastaa wakubwa wamekuwa wakiteswa sana na kiki na zimekuwa kikwazo kikubwa kwao,” alisema Baby Madaha anayetamba na Ngoma ya Mjanja Wangu.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment