Search This Blog
Sunday, August 4, 2019
Ahukumiwa kwenda jela kwa kutoa lugha chafu dhidi Rais Museveni
Mwanaharakati msomi nchini Uganda, Dkt. Stella Nyanzi amehukumiwa kwenda jela mwaka mmoja na nusu kwa kosa la kumtolea lugha chafu Rais wa nchi hiyo, Yoweri Kaguta Museveni.
Nyanzi amekutwa na hatia ya unyanyasaji wa kimtandao pamoja na mawasiliano ya udhalilishaji dhidi ya rais Yoweri Museveni na familia yake.
Aidha, kabla ya hukumu hiyo, Dkt. Nyanzi alikataa kumsikiliza hakimu wakati akisoma hukumu dhidi yake na badala yake kufanya vurugu kwa kuvua nguo na kuonesha sehemu ya mwili wake.
Wakati kesi ikiendelea, Dkt. Nyanzi alikataa kuomba dhamana na amekuwa katika gereza kuu la Uganda la Luzira kwa miezi minane tangu akamatwe.
Pia Dkt. amekuwa mtu maarufu sana nchini humo ambaye amekuwa akitumia lugha chafu kuukosoa hadharani utawala wa Rais Museveni kwa kuandika katika mitandao ya kijamii maneno yasiyokuwa na staha kuhusu utawala wa Rais huyo.
Dkt. Nyanzi ambaye ni mtafiti wa masuala ya jamii, kabla ya kuanza kampeni yake ya matusi kupitia kwenye mitandao ya kijamii aliwahi kuwa mhadhiri katika chuo kikuu cha umma nchini Uganda cha Makerere.
Sudan: Mauaji ya wanafunzi yapelekea shule kufungwa nchi nzima
Zimbabwe yakerwa na vikwazo vya Marekani dhidi balozi wake nchini Tanzania
Serikali ya Msumbiji na wapinzani wasaini mkataba wa Amani
Hata hivyo, mashtaka hayo chini ya sheria ya matumizi mabaya ya kompyuta ni jaribio la utekelezwaji wa sheria ya uhalifu wa mtandaoni inayokosolewa na wengi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment