Search This Blog

Tuesday, July 23, 2019

Wadiwani walia na nyongeza ya Posho


Mkutano Mkuu wa 35 ALAT Taifa unaendelea jijini Mwanza huku Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa akitarajiwa kuuzindua rasmi baadaye ukiwa ni mkutano wa siku tatu ulioanza jana Jumatatu, Julai 22.

Katika salaam za awali za Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu ambaye pia ni Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Mwanza, Hilali Elisha amemuomba waziri mkuu kuangalia upya waraka uliopunguza posho za madiwani.

Amesema kuwa katika waraka huo yalitolewa maelekezo ya kupunguzwa kwa posho hizo hadi kufikia Shilingi 40,000 kwa kikao na kufuta malipo ya nauli za madiwani kitendo kilichowafanya madiwani hao kuishi kwa shida na kupunguza kasi ya kuwaletea maendeleo wananchi.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...