Search This Blog

Thursday, July 4, 2019

Tetesi: Leicester City yatenga Tsh. Bilioni 40 kumnasa Mbwana Samatta


Klabu ya Leicester City imetuma ofa inayokadiriwa kufikia Bilion 40 za Kitanzania kwa ajili ya mfungaji bora wa klabu ya KRC Genk, Mbwana Samatta.

Vyanzo mbalimbali kutoka England vimeripoti kuwa vigogo wanapigana vikumbo kupata saini ya mshambuliaji huyo wa Kitanzania. Mapema wiki hii klabu ya Cardiff ilipeleka dau la Tsh. Bilion 36 likatupiliwa mbali na Genk.

Klabu za Birmingham na Aston Villa pia zimepeleka ofa ya Tsh. Bilion 40 lakini vilabu hivi vimekutana na kizingiti kingine lakini maofisa wa Leicester wamejitosa katika dili hili.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...