Search This Blog
Sunday, July 21, 2019
Sijaona wala kusikia malalamiko ya akina Kinana - Polepole
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amesema hajaiona nakala ya barua ya malalamiko ya kudhalilishwa iliyowasilishwa na makatibu wakuu wawili wastaafu wa chama hicho, Yusuf Makamba na Abdulrahman Kinana.
Polepole Jumapili kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi kupitia mtandao wa WhatsApp kuwa hajasikia malalamiko hayo kwa kuwa kwa sasa yupo kwenye ziara vijijini.
Wakati Polepole akisema hajasikia malalamiko hayo ambayo si tu yameandikwa na vyombo vya habari, waraka wake pia umesambaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwamo WhatsApp na hivyo kuzua mjadala mkubwa kabla na baada ya baadhi ya wabunge wa chama hicho kuendelea kujitokeza kila siku kuwajibu wastaafu hao.
Polepole ambaye alitafutwa na gazeti hili kwa ajili ya kupata ufafanuzi wa CCM kuhusu barua hizo na hatua ambazo itachukua dhidi ya malalamiko ya viongozi hao wastaafu wa chama hicho, alisisitiza kuwa atakapoiona atatujuza.
Jumapili iliyopita Makamba na Kinana walimwandikia barua Katibu wa baraza la ushauri la viongozi wakuu wastaafu wa CCM, Pius Msekwa wakilalamika kudhalilishwa kwa mambo ya uzushi na uongo na mtu anayejitambulisha kama mwanaharakati na mtetezi wa serikali na kushangaa chama hicho kukaa kimya.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment