Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo amezungumzia suala la kugombea Ubunge katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2020.
Akizungumza na EA Radio, Prof. Mkumbo amesema kuwa kwa sasa anatekeleza majukumu aliyokabidhiwa na Rais Magufuli kuhakikisha kuwa maji yanatoka maeneo mbalimbali nchini na ikifika wakati husika ataamua endapo atagombea ama vinginevyo.
"Suala la Ubunge kwa sasa bado, ninachapa kwanza kazi aliyonikabidhi Rais Magufuli. Imebaki miezi 12 ya kujua hatma na maamuzi ya endapo nitagombea ama vinginevyo", amesema Prof. Mkumbo.
Pia amezungumzia juu ya kero sugu za maji zinazosumbua maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam kama Gongo la mboto, Chanika, Goba na maeneo mengine ambayo miradi haijakamilika, ambapo amesema mchakato wa kukamilisha miradi hiyo unakwenda kwa kasi na ndani ya miezi 12 ijayo wananchi wataanza kutumia maji.
"Wananchi wa Dar es salaam na maeneo mengine nchini wasiwe na wasiwasi, serikali inaendelea kutekeleza ilani ya CCM kwa ufanisi, mpaka kufikia April mwaka huu tumeweza kuwasambazia maji wanannchi kwa asilimia 65 na malengo yetu mpaka mwisho wa 2020/21 tutakuwa tumewafikia wananchi kwa asilimia 85", ameongeza.
Profesa Kitila Mkumbo alikuwa mshauri wa Chama cha ACT-wazalendo kabla ya kuteuliwa na Rais Magufuli, April 04, 2017 kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji ambayo bado anahudumu mpaka sasa
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment