Search This Blog
Tuesday, July 2, 2019
Makamu wa Rais awataka wafanyabiashara kutotegemea kuuza nje bidhaa
Jumuiya ya wafanyabiashara watakiwa kutoendelea kutegemea kuuza nje bidhaa ghafi bali watumie viwanda vya nyumbani na bidhaa hizo ziongezwe thamani kwa kusindikwa na kufungashwa kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.
Ameyasema hayo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu katika sherehe za ufunguzi wa Maonesho ya 43 ya biashara ya Kimataifa yaliyofanyika katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Wanahabari katika sherehe hizo Mh. Samia amesema kuwa jumuiya ya wafanyabiashara ina jukumu la kuwandaa wanachama wake kuwa na ufahamu wa kutosha, kuwa na uthubutu na kutayarisha miradi na kuwa tayari kupambana katika medani ya biashara.
“Ili Tanzania iweze kukidhi mahitaji ya fursa za masoko ya biashara zao, tunahitaji kufanya kazi kwa bidii kwa kuzalisha bidhaa zenye ushindani”. Amesema Mh. Samia.
Aidha, Samia amesema kuwa ili ujenzi wa Uchumi wa Viwanda ushike kasi ya kutosha, hakuna budi kwa sekta kama kama vile kilimo, mifugo,Uvuvi na madini kutoa malighafi za kutosheleza viwanda hivyo.
“Wakati tunahimiza ujenzi wa Uchumi wa Viwanda msukumo tunauweka pia kwenye sekta zinazozalisha malighafi.Sekta ya kilimo ikijipanga vema, viwanda vitapata malighafi hivyo hivyo kwa sekta ya mifugo, uvuvi, madini na sekta nyingine”. Ameongeza Mh. Samia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment