Search This Blog

Sunday, June 9, 2019

Waandamanaji waanzisha kampeni dhidi ya jeshi Sudan

Kundi la waandamanaji linaloongozwa na taasisi ya wanataaluma nchini Sudan, hapo jana lilitangaza kampeni ya uasi wa kiraia wa nchi nzima hadi hapo utawala wa kijeshi utakapokabidhi madaraka kwa serikali ya kiraia.

Kampeni hiyo iliyotangazwa kuanza rasmi leo, imeitishwa muda mfupi baada ya waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed kuitembelea Sudan, kwa lengo la kufufua mazungumzo kati ya viongozi wa waandamanaji na baraza la mpito la kijeshi.

Hayo yanaendelea ikiwa ni masaa kadhaa tangu kukamatwa kwa baadhi ya viongozi wakuu wa upande wa upinzani ambao pia walihudhuria mazungumo na waziri mkuu wa Ethiopia. Sudan imekuwa katika hali ya sintofahamu tangu ulipoingia madarakani uongozi wa kijeshi, mara baada ya kung'olewa kwa aliyekuwa Rais wa zamani wa nchi hiyo Omar Al Bashir.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...