Search This Blog
Wednesday, June 26, 2019
Unaambiwa Watumiaji DAWA za Kulevya Wapungua Tanzania
Tanzania imeungana na mataifa mengine duniani leo Juni 26, kuadhimisha siku ya kimataifa ya kupambana na matumizi na biashara ya dawa za kulevya, ikiwa ni nchi mwanachama wa umoja wa mataifa.
Maadhimisho hayo yamefanyika kitaifa mkoani Tanga yakiwa na kauli mbiu “Waathirika wa dawa za kulevya wana haki ya kupata huduma za afya” lengo likiwa ni kuikumbusha jamii juu ya uelewa wa wimbi la biashara na matumizi ya dawa za kulevya.
Kutokana na Serikali kuendelea kusimamia utoaji tiba kwa waathirika wa dawa za kulevya ili kupunguza madhara yanayotokana na matumizi ya dawa hizo, na kufanikiwa kupunguza idadi ya waathirika wa dawa za kulevya katika vituo vya tiba kutoka wagonjwa 2,400 mwaka 2015 hadi wagonjwa 700 mwaka 2018.
Hali iliyosaidia kupunguza maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa waraibu wa dawa za kulevya wanaojidunga kutoka 35% mwaka 2015 hadi 18.5% mwaka 2018.
Mbunge wa Kenya aliyetaka wafanyabiashara Watanzania wafukuzwe akamatwa
Ikumbukwe kuwa matumizi ya dawa za kulevya husababisha madhara kiafya ikiwa ni pamoja na kuchochea kuenea kwa maambukizi ya vurusi vya UKIMWI, virusi vya homa ya ini aina B na C,kifua kikuu, magonjwa ya akili pomoja na usugu wa tiba ya kifua kikuu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment