Search This Blog
Saturday, June 8, 2019
Sarah wa Harmonize ashindwa kupanda mlima huko Mtwara
Huwezi kuamini!!! Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Harmonize kutoka WCB, amejikuta akimbeba mgongoni mpenzi wake Sarah baada ya kushindwa kupanda Mlima Mkomaindo ulioko mkoani Mtwara.
Tukio limetokea wakati msanii huyo akiwa mjini ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa Masasi Rock Festival, lililoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
Wakati wa kupanda mlima huo, Sarah ambaye ni raia wa Italy, alionekana kuchoka na kushindwa kuendelea ambapo katika hali isiyotegemewa na wengi Harmonize ambaye ni mwenyeji wa Mtwara alimbeba mgongoni na kuwaacha watu waliokuwapo hapo kuangua vicheko.
Tamasha hilo linatarajiwa kuisha Juni 9, mwaka huu likiwa na lengo la kutangaza utalii wa ndani ya mkoa wa Mtwara. Kaulimbiu ya Tamasha hilo ni ‘Tukutane Kileleni.’
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment