Search This Blog
Monday, June 24, 2019
Rwanda yapokea Faru Weusi kutoka Ulaya
Faru watano walio kwenye hatari kubwa ya kutoweka wamepokelewa na Rwanda kutoka Ulaya. Kwa mujibu wa Bodi ya maendeleo ya Rwanda faru hao watatunzwa katika mbuga ya taifa ya Akagera, iliyoko mashariki mwa Rwanda.
Hatua hiyo inatokana na jumuiya ya bustani za wanyama ya Ulaya, serikali ya Rwanda na shirika lisilo la kiserikali la African Parks, inayosimamia mbuga ya wanyama ya Akagera pamoja na bodi ya maendeleo ya Rwanda.
Mkuu wa idara ya hifadhi ya Bodi ya Maendeleo ya Rwanda Bw. Eugene Mutangana, amesema faru hao kuhamishiwa Rwanda kutahimiza sekta ya utalii, ambayo huiingizia mapato serikali ya Rwanda.
Wanyama hao walikusanywa mwaka jana kutoka kwenye bustani kadhaa za wanyama kutoka Ulaya kabla ya kusafirishwa kwenda Rwanda.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment