Search This Blog
Tuesday, June 11, 2019
RC Katavi atoa onyo kali kwa Wanasiasa
Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Juma Homera amesema licha ya kutafsiriwa vibaya kwenye baadhi ya vyombo vya habari, hatasita kuchukua hatua kwa watu wote wanaofanya kampeni za kupita nyumba kwa nyumba kuwashawishi wananchi kwa lengo la kufanikisha mambo yao ya siasa.
Juma Homera ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali waliomtembelea ofisini kwake kwa lengo la kujua mikakati na mipango ya maendeleo ya mkoa huo katika kuwaletea maendeleo wananchi.
“Nawaonya wananchi hususani wanasiasa kuacha kufanya siasa za nyumba kwa Nyumba kwa sababu muda wa siasa hizo bado na msajiri wa vyama vya siasa alishapiga marufuku mikutano hiyo kasoro ile ya ndani tu ,vinginevyo sheria itachukua mkondo wake.
Homera amesema marufuku hiyo ni kwa vyama vyote vya kisiasa nchini ikiwemo CCM na vyama vingine vyote vya siasa.
“Hii ni Juni,wanasiasa wakae wasubiri muda mwafaka ufike wafanye wanachokifanya na tena ni kwa mujibu wa sheria,si kiholelaholela,” amesema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment