Search This Blog

Monday, June 10, 2019

Mwadui FC kusuka kikosi kipya


Uongozi wa Mwadui FC umesema kuwa kwa sasa hesabu zao ni kusuka kikosi kipya kitakacholeta ushindani mkali msimu ujao baada ya kubaki kwenye Ligi Kuu Bara.

Katibu wa Mwadui, Ramadhan Kilao amesema kuwa baada ya kubaki kwenye ligi mpango wa kwanza ni kusuka kikosi upya.

"Tumenusurika kushuka daraja kutokana na kushindwa kumudu ushindani kwa msimu uliopita, kwa sasa tunaangalia namna bora itakayotufanya tuwe bora kwenye ushindani msimu ujao.

"Kikosi makini na chenye nguvu tutakuwa nacho msimu mpya hivyo mashabiki na wadau waendelee kutupa sapoti kama ambavyo walikuwa nasi bega kwa bega kwenye mchezo wetu wa playoff dhidi ya Geita," amesema.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...