Search This Blog

Sunday, June 2, 2019

Mitandao ya kijamii ya wanaotaka kwenda Marekani kuchunguzwa


Wote wanaotuma maombi ya kupata Visa kueleka nchini Marekani sasa watahitajika kutoa majina yao ya mitandao ya kijamii, anwani zao na nambari za simu katika sheria mpya zilizowekwa.

Kulingana na sheria mpya za idara ya maswala ya kigeni, wanaotuma maombi ya Visa watahitajika kutoa majina yao ya mitandaoni mbali na anwani za miaka mitano pamoja na nambari za simu.

Wakati sheria hiyo ilipopendekezwa mwaka jana, mamlaka ilikadiria kwamba itaathiri takribani watu milioni 14.7 kila mwaka.

Hatahivyo baadhi ya wanadiplomasia na maafisa wanaotuma maombi ya kibali hicho huenda wakasamehewa.

Hatahivyo watu wanaoelekea Marekani kufanya kazi ama kusoma watalazimika kutoa habari zao .

''Tunajaribu kutafuta mikakati ya kuimarisha ukaguzi wetu ili kuwalinda raia wa Marekani , huku tukiunga mkono wale wanaosafiri kihalali'' , ilisema Idara hiyo.

Awali , ni watumaji maombi waliohitaji ukaguzi wa zaidi -kama vile watu waliosafiri katika maeneo yanayodhibitiwa na magaidi -ambao wangelzimika kutoa data hiyo.

Lakini asasa wanaotuma maombi watalazimika kutoa majina ya akaunti zao katika mitandao ya kijamii, mbali na kutoa maelezo ya akaunti zao katika mtandao yoyote.

''Mtu yeyote atakayedanganya kuhusu matumizi yao ya mitandao ya kijamii huenda akakabiliwa na adhabu kali ya uhamiaji'', kulingana na afisa aliyezungumza na The Hill.

Rais Donald Trump
Utawala wa rais Donbald Trump ulipendekeza sheria hizo mnamo mwezi Machi 2018.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...