Search This Blog
Tuesday, June 11, 2019
Iringa wasalimisha Kilo 344 za mifuko ya Plasitiki
Wafanyabiashara mbalimbali wilayani Mufindi mkoani Iringa wamesalimisha jumla ya kilo 344 za mifuko ya Plasitiki kwa ajili ya kuteketezwa ikiwa ni sehemu ya kutekeleza agizo la serikali la upigaji marufuku matumizi ya mifuko hiyo.
Akikabidhi mifuko hiyo kwa mkuu wa mkoa wa Iringa, Alli Hapi jana wakati wa madhimisho ya siku ya mazingira duniani iliyofanyika katika viwanja vya mashujaa mjini Mafinga wilani Mufindi kwa mkoa wa Iringa, mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Wiliam alisema kuwa mifuko hiyo imesalimishwa katika ofisi za Halmashauri na wafanyabiashara hao kabla kuanza kwa utekelezaji wa agizo la serikali na uzuiaji wa matumizi ya mifuko hiyo.
Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa wilaya ya Mufindi iliweza kutoa elimu kwa wananchi wake juu ya zuio la matumizi ya mifuko hiyo na hadi sasa wananchi wameanza matumizi ya mifuko mbadala inayotengenezwa na vikundi vya wajasiriamali kutoka ndani ya wilaya hiyo kwa kutumia karatasi kutoka kiwanda cha Mgololo kilichopo wilayani hapo .
”Wananchi wetu wa Mufindi wameheshimu sana na kupokea maelekezo ya serikali ya kuanza matumizi ya mifuko mbadala lakini mkuu wa suala hili la mazingira ni pana sana na linagusa maisha ya wananchi wetu tunajua suala la kutunza vyanzo vya maji tumekuwa tukilipigia kelele na suala hili bado lipo na tumekuwa tukiwapigia kelele wananchi wetu kuhakikisha wanaacha hatua tano kutoka mito pindi wanapofanya shughuli za kilimo.”
Kwa upande wake, Mkuu wa mkoa wa Iringa, Ali Hapi mbali ya kupongeza hatua iliyochukuliwa na wafanyabiashara na watumiaji wa mifuko ya plastiki wilayani Mufindi kwa kukabidhi kilo 344 za mifuko hiyo kwaajili ya kuteketezwa bado aliziagiza halmashauri zote za mkoa wa Iringa kuendelea kutoa elimu na kuwachukulia hatua wale wote ambao wanatumia mifuko ya plastiki mweupe kwa kufungashia bidhaa ambazo hazijawekewa nembo ya ubora na TBS.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment