Search This Blog

Saturday, June 15, 2019

Baba Aliwaua Watoto Wake Watano Ahukumiwa Kunyongwa

Baba aliyewaua watoto zake watano nchini Marekani amehukumiwa kunyongwa mpaka kufa, mahakama imeamua na kutupilia mbali ombi la msamaha la mama wa watoto hao.

Mama wa watoto hao Amber Kyzer, aliiambia mahakama siku ya Jumanne kuwa, baba huyo Tim Jones Jr, 37 ambaye alishakutwa na hatia ya mauaji, "Hakuonesha huruma hata kidogo kwa watoto. Kama ningeweza ningemrarua uso wake hata sasa... lakini watoto wangu walimpenda."

Hukumu hiyo imetolewa baada ya waendesha mashtaka kudai kuwa, hukumu ya kifungo cha maisha jela itakuwa ni sawa na "kumpeleka Timmy chumbani kwake."


Hukumu hiyo imetolewa na mahakama ambayo ilimtia hatiani bwana huyo kwa mauaji ya watoto hao waliokuwa na mwaka mmoja mpaka miaka minane mwaka 2014.


Mama wa watoto hao Amber Kyzer aliiomba mahakama isimuue baba huyo
Wazee wa baraza wa mahakama hiyo, wanaume saba na wanawake watano walitakiwa kufikia uamuzi wa pamoja, na laiti wangetofautana Jones angehukumiwa kifubgo cha maisha jela.

Wazee hao wa baraza walikubaliana kuhusu hukumu hiyo baada ya saa mbili za majadiliano.

Je, bado biharusi anachunguzwa iwapo ni bikira?
Katika mijadala ya kisheria juu ya hukumu hiyo, waendesha mashtaka waliwataka wazee wa baraza kukumbuka ni kwa namna gani bwana huyo aliwaua watoto.

Jones alikiri kuwa alimfanyisha mazoezi magumu mtoto wake mkubwa mpaka akadondoka na kufariki.

Baada ya hapo aliwanyonga wanne waliosalia mmoja baada ya mmoja, na kupakia miili yao kwenye gari na kuliendesha kwa siku tisa, kabla ya kuitupa kwenye matanki ya takataka kwenye jimbo la Alabama.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...