Search This Blog
Sunday, June 23, 2019
Baada ya Harmonize, Vanessa Mdee naye kufanya yake
Msanii nyota wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee anajiandaa kuachia E.P yake (nyimbo chache zinazounganishwa pamoja) ambayo ameiita Expensive.
Katika uthibitisho wa hilo, ametuonesha Cover art ya EP hiyo ambayo inatarajiwa kutoka hivi karibuni. Habari njema ni kwamba ndani ya EP hiyo pia Vanessa ana Collabo na mdogo wake Mimi Mars.
Tayari Mimi Mars alithibitisha ujio wa Collabo hiyo akiwa kwenye mahojiano na kituo kimoja cha redio hapa nchini mwezi mei mwaka huu na pia alisema Collabo hiyo ndiyo iliyobeba jina la EP hiyo.
Vanessa Mdee atakuwa msanii wa pili kutoka kwenye Bongo Fleva kwa mwaka huu kuachia EP baada ya Harmonize aliyeachia ya kwake inayokwenda kwa jina la Afro Bongo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment