Search This Blog

Wednesday, May 29, 2019

Upinzani Sudan waandaa mgomo


Muungano wa upinzani nchini Sudan pamoja na makundi ya waandamanaji, wameshiriki mgomo kulishinikiza baraza la jeshi kuachia madaraka utawala wa kiraia.

Wahudumu wa afya, umeme na wafanyakazi wa benki walishiriki mgomo huo na katika sekta nyingine shughuli ziliathiriwa kidogo.

Kufuatia mgomo huo, baadhi ya mashirika ya ndege yalisitisha safari zao kutoka uwanja wa ndege wa Khartoum.

Shirika la habari la AFP limeripoti kuwa mamia ya wasafiri walikwama katika uwanja wa ndege mjini Khartoum na katika baadhi ya vituo vya mabasi.

Kama hatua ya kuongeza shinikizo dhidi ya baraza la kijeshi linaloshikilia madaraka kwa sasa, vuguvugu linaloendesha maandamano kwa jina Freedom and Change, limeitisha mgomo wa kitaifa wa siku mbili kuanzia leo.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...